Diamond Amaliza ziara ya Ulaya, Adai Reality TV Show yake itaweka Wazi Mambo Mazito

Diamond Platnumz amemaliza ziara yake ya Ulaya aliyoipa jina, From Tandale to The World Tour iliyompeleka kwenye nchi takriban nane.
Show yake ya mwisho ilifanyika Jumamosi hii jijini Copenhagen, Denmark ambayo video zake inaonesha ilikuwa na mafanikio makubwa.
Mchumba wake Zari aliyemsindikiza kwenye nchi zote alizopita, ameshukuru kwa kuandika: Allow me to thank everyone that helped us while out there in Europe. For showing us around and hosting us. Mostly thank you for allowing my hubby entertain you. Stay blessed.
Tayari Zari amerejea Afrika Kusini kuungana na familia yake.

Katika hatua nyingine Diamond amedai kuwa reality TV show yake ijayo itaweka wazi mambo mengi mazito.

“Can you try to guess the name of our Reality Show?) (Muda si Mwingi Kipindi cha Maisha yangu ya kila siku, Familia na Team yangu nzima itaanza kuwa kwa Tv yako pendwa, ” ameandika Instagram.

“Nakuahidi sio tu eti Kireality show … ni Reality show Bora ambayo naamini utaipenda kunzia kwenye Quality, Mikasa na matukio yote nnayopitia mimi, Familia na Team yangu kila siku….Mengi yanaonekana, Unayoyasikia, Unayasoma ila kwenye Hiki kipindi ndio itakuwa Thibitisho la kila uvumi uusikiao….Sjui Kipini puani, Mara jicho, Mara sjui @officialshetta , Mara DNA, Mara @romyjons kutoinekana tena kwenye Tour Ghafla….Niamini mimi yote utaona na kuyapata kwa uwazi kabisa, Kaa na Mimi…….! We unavyohisi reality Show yetu itakuwa inaitwaje…..?” ameongeza.
Previous
Next Post »